Wakazi wapatao 36,263 wa vijiji 7 watanufaika na huduma ya maji safi na salama kufuatia ujenzi wa mradi wa maji utakaogharimu zaidi ya shilingi Bilioni 6.9
Mradi huo ambao umeanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2023/2024 tarehe 07/03/2024 utawanufaisha wakazi 32,641 kutoka katika vijiji vya kata ya Kibirashi na 3,622 kutoka kijiji kimoja katika kata ya Kisangasa.
Vijiji vya kata ya Kibirashi ambavyo wakazi wake watanufaika na mradi huo ni Nkoa Kibirashi,Kwamaligwa,Gombero,Elerai na Gitu ambapo kwa upande wa kata ya Kisangasa kijiji ambacho wakazi wake watanufaika na mradi huo ni Kwediswati
Mradi huo ambao umewekewa jiwe la msingi na kiongozi wa kitaifa wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 ndugu Ismail Ali Ussi tarehe 07/06/2025 utekelezaji wake umefikia asilimia 50 ukihusisha kazi za ujenzi wa kidakio/intake (50%),ujenzi wa ki banda cha mitambo(70%),ujenzi wa njia ya umeme(60%),ujenzi wa matenki ya maji yenye mita za ujazo1,000 na 300 (50%).
Kazi nyingine ni ununuzi wa bomba uchimbaji mtaro,ulazji na uunganishaji bomba umbali wa mita 49,265 (60%),ujenzi wa vituo vya kuchotea maji 47 (20%),ununuzi na ufungaji wa pampu ya kusukumia maji (0%),ujenzi wa ofisi ya usimamizi wa mradi-CBWSOs (0%) na ujenzi wa uzio kuzunguka kibanda cha mitambo na tanki za maji (0%)
Mradi ulitarajiwa kukamilika tarehe 06/04/2025 lakini kutokana na sababu mbalimbali mradi huu sasa unatarajiwa kukamilika tarehe 01/09/2025 na hadi utakapokamilika utasaidia wilaya kuwa na ongezeko la asilimia 9.7 la wananchi wanaopata huduma ya maji safi na salama
Shukrani kwa serikali inayoongozwa na Mh:Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha wananchi wanapata huduma muhimu kama maji karibu na maeneo yao na kutekeleza azma ya kumtua mama ndoo kichwani kwa vitendo.
MWISHO
Copyright ©2018 Kilindi DC . All rights reserved.