• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kilindi District Council
Kilindi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara
        • Elimu Msingi
        • Elimu Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maendeleo ya Jamii
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Ardhi na Maliasili
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Shughuli za Mifugo na Uvuvi
    • Shughuri za Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji na Umwagiliaji
    • Huduma za Kilimo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu na Majukumu yake
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Mradi wa Maji
      • Miradi ya Afya
    • Miradi inayoendelea
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
    • Miradi iliyokamilika
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video Mbalimbali

ILANI YA CCM YATEKELEZWA KWA VITENDO WILAYANI KILINDI.

Posted on: November 23rd, 2022

Serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 429,720,000/= kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Songe ikiwa ni utekelezaji kwa vitendo wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ili kuondoa kero za wananchi wake.

Akiwasilisha utekelezaji wa  Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa kipindi cha Julai 2021 hadi Septemba 2022 Mkuu wa wilaya Kilindi Mh:Abel Yeji Busalama alisema mradi wa ujezi wa daraja hili ni miongoni mwa miradi iliyofanyika katika robo ya kwanza ya mwaka 2022/2023.

Alisema ujenzi wa daraja la Songe umewezesha kutatua kero ya wananchi na wasafiri kushindwa kupita wakati wa mvua kubwa kwani maji  wakati mwingine yanapozidi husababisha watu na vyombo vya usafiri kushindwa kupita hadi yapungue

Alisema serikali wilayani Kilindi inatoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh:Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo amekuwa akitekeleza kwa vitendo ilani ya Chama kwa kutatua kero za wananchi ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara na kumtaja Mkandarasi wa ujenzi wa daraja la Songe kuwa ni Motosach International

Akitaja mradi mwingine uliotekelezwa katika robo ya 2022/2023 Mh:Busalama alisema ni matengenezo  ya barabara ya Songe Mjini kwa kiwango cha Lami (Mita 300),mradi uliotengewa kiasi cha shilingi 243,124,600/= unaotekelezwa na  Mkandarasi JP Traders.

Akifafanua zaidi alisema miradi mingine ya ujezni wa miundombinu ni ujenzi wa daraja la Chamata (Lwande) ambao serikali ilitoa kiasi cha  shilingi 984,870,500/= na Mkandarasi wa mradi huu ni Gloda Construction Co Ltd

Mradi mwingine uliotekelezwa katika robo ya kwanza ya 2022/2023 ni ujenzi wa daraja la Lusane kwenye barabara ya Tunguli (Msamvu)-Kibati ambao ulitengewa kiasi cha shilingi 124,000,000/=na kumtaja Mkandarasi wa mradi huu ni ATMO Constractors Ltd,na kuongeza kuwa  miradi hii yote ya ujenzi wa miundombinu ilitekelezwa na TANROAD.

Akielezea miradi iliyotekelezwa na wakala wa barabara wa Vijijini na Mijini (TARURA) Mh:Busalama alisema wilaya imeendelea kuhakikisha miundombinu ya barabara inaboreshwa kama ilivyoelekezwa katika ibara ya 56 ya ilani ya uchaguzi ya CCM 2020-2025.

Alisema TARURA wilayani Kilindi inahudumia jumla ya kilomita 871.59 na kwa mwaka 2021/2022 TARURA Kilindi ilipokea Tsh 1,038,153,784.47/= za Mfuko wa barabara (Road Fund),Tsh 500,000,000/=za mfuko wa jimbo (450,000,000/= zililetwa) na Tsh 1,000,000,000/= za Tozo (849,194,771.08 zililetwa)

Alisema katika mwaka wa fedha 2022/2023 TARURA Kilindi imepangiwa Tsh 980,113,478,.26/= za Mfuko wa barabara (Road Fund) na hadi mwisho war obo ya kwanza hapakuwa na fedha zilizopokelewa.

Mh:Busalama alisema  ujenzi wa miundombinu ya barabara ni utekelezaji wa Ilani ya CCM 2020-2025 ibara ya 55, ambayo imeiagiza serikali kuendeleza shughuli za ujenzi wa mindombinu mbalimbali na kuongeza kuwa utekelezaji wa miradi yote ya ujenzi wa miundombinu wilayani Kilindi ni kuhakikisha wananchi wanaondokana na tatizo la ukosefu wa miundombunu kwa ajili ya shughuli zao za maendeleo.

Akizungumzia huduma mbalimbali za kilimo zilizotekelezwa katika mwaka wa fedha 2021/2022Mh:Abel Yeji Busalama alisema jumla ya tani 33,840 za Mkonge ziligawiwa kwa wananchi wa kata za Msanja,Jaila na shule ya msingi Mgambo

Alisema lengo la kusambaza mbegu hizo ni ukinua kilimo cha Mkonge katika mkoa wa Tanga na hatimaye kuinua uchumi wa wananchi kupitia kilimo hicho.

Alisema sanjari na hilo serikali ilifanikwa kugawa kilo 2,397 za mbegu za Alizeti kwa wakazi wa kata za Bokwa,Kilwa na Msanja ambapo kwa zao la Maharagwe jumla ya kilo 2100 ziligawiwa katika kata za Kilindi,Pagwi,Songe,Bokwa,Mvungwe,Kibirashi na Masagalu

Akizungumzi sumu za viwavijeshi jumla ya lita 3648 zilitolewa na serikali kisha kugawiwa katika kata za Kwekivu,Tunguli,Lwande,Mabalanga,Kibirashi,Kilwa,Mkindi,Negero,Masagalu,Songe,Bokwa,Mvungwe,Kimbe,Msanja,Kisangasa,Kwediboma na Saunyi.

Mh:Busalama alisema zao la Korosho nalo halikuachwa kwani serikali katika mwaka 2021/2022 ilifanikiwa kutoa kilo 185 za mbegu  na kuzigawa katika kata za Kilindi,Mvungwe,Kibirashi,Songe,Bokwa,Msanja na Mkindi na kwa zao la Mpunga serikali ilitoa kilo 1200 za mbegu na kuzigawa katika kata za Negero,Lwande,Kilindi,Kibirashi,Kilwa na Kimbe.

Mh:Busalama alisema ibara ya 37(B) (d) ya Ilani ya CCM inaagiza kuongeza uzalishaji na tija kwa mazao ya chakula na kuongeza utoshelevu wa chakula hivyo utoaji wa huduma zote katika kipindi cha utekelezaji kwa mwaka 2021/22 ni utekelezaji wa ilani ya chama kwa vitendo.

MWISHO

Na Modi Mngumi-Kilindi

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI WILAYA YA KILINDI KWAAJILI YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA MWAKA 2024 September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA ZA JESHI LA MAGEREZA February 01, 2024
  • TANGAZO LA CHAGUZI NDOGO ZA UDIWANI KUTOKA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZA (NEC) February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA April 17, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MH: WAZIRI ULEGA AFANYA ZIARA NA KUKAGUA UJENZI WA BARABARA WILAYA KILINDI

    January 05, 2025
  • WAKAZI WA MGERA WALIOJENGA KANDO YA MTO LUKIGULA WATAKIWA KUONDOKA

    December 20, 2024
  • JAMII ITOE KIPAUMBELE ULAJI WENYE MAKUNDI YOTE MUHIMU YA VYAKULA

    December 12, 2024
  • HALMASHAURI YA WILAYA KILINDI YATOA MIKOPO YA SHILINGI MILIONI 569,850,000.00

    November 18, 2024
  • Tazama zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda S.Mtondoo alipotembelea Mgodi wa Dhahabu wa Seita
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Hati ya Mishahara
  • SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO TANZANIA, 2015
  • SERA YA TEHAMA YA TAIFA YA MWAKA 2016
  • SHERIA YA MIAMALA YA KIELEKTRONIKI YA MWAKA 2015
  • SHERIA YA MAWASILIANO YA KIELEKTRONIKI NA POSTA 2010
  • KITENGO CHA MUITIKIO WA DHARURA WA MATUKIO YA MITANDAONI
  • Mfumo wa Mpango na Bajeti
  • Mfumo wa ffars
  • Mwongozo wa Kutumia Mfumo wa FFARS

Tovuti Nyingine

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • Baraza la Taifa la Elimu ya kiufundi
  • Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala bora
  • Tovuti ya Ikulu
  • TUME YA TAIFA YA UKIMWI TANZANIA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Copyright ©2018 Kilindi DC . All rights reserved.