• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kilindi District Council
Kilindi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara
        • Elimu Msingi
        • Elimu Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maendeleo ya Jamii
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Ardhi na Maliasili
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Shughuli za Mifugo na Uvuvi
    • Shughuri za Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji na Umwagiliaji
    • Huduma za Kilimo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu na Majukumu yake
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Mradi wa Maji
      • Miradi ya Afya
    • Miradi inayoendelea
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
    • Miradi iliyokamilika
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video Mbalimbali

Wilaya Ya Kilindi Yavuka Malengo Ya Upandaji Miti Kitaifa.

Posted on: May 22nd, 2019

Wilaya ya Kilindi imepanda jumla ya miti 1,975,000 ikiwa ni sawa na asilimia 131.66 ukilinganisha na lengo la Kitaifa la kupanda miti 1,500,000 kwa kila Wilaya kwa mwaka 2017/2018.

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda Mtondoo ameyasema hayo alipo kuwa akizindua wiki ya upandaji miti Wilaya ya Kilindi. Uzinduzi huo umefanyika katika shule ya Msingi Kwamwande iliyopo ndani ya kata ya Bokwa.

Aidha katika kutekeleza hayo Wilaya ya Kilindi iliweka lengo la kupanda miti 1,983,000 ili kuhakikisha inarejesha uoto wa asili kwa haraka, hata hivyo miti yote ilipandwa lakini kulingana na changamoto mbalimbali miti 1,975,000 pekee ndiyo iliyomea ikiwa ni sawa na asilimia 99.6 kwa malengo ya Wilaya.

Hivyo mkuu wa Wilaya aliwapongeza viongozi wa vijiji, kata na Wilaya kwa utekelezaji wa agizo hilo. Nakuwasihi waendelee kuhakikisha wanatunza mazingira na kudhibiti vitendo vyote vya uharibifu wa mazingira ikiwa ni pamoja na kukata miti hovyo.

Kwa mwaka 2018/2019 Wilaya ya Kilindi imeweka lengo la kupanda jumla ya miti 1,959,000. Hivyo Mhe. Mtondoo amewataka viongozi wa vijiji kutunga na kusimamia sheria ndogo zitakazo hakikisha kila kaya inapanda miti isiyopungua mitano, lakini pia maeneo ya taasisi ikiwa ni pamoja na Shule na Zahanati zilizopo katika kila kijiji.

“Watendaji wote wa kata mhakikishe mnatoa taarifa za utekelezaji kabla ya tarehe 25.06.2019” alisema hayo Mhe. Mtondoo alipokuwa akisisitiza umuhimu wa wananchi kutunza mazingira yanayowazunguka kwa kupanda miti.

Naye Diwani wa Kata ya Bokwa Mhe. Idrisa Mgaza ameushukuru uongozi wa Wilaya kwa kufanya uzinduzi huo katika shule ya Msingi Kwamwnde ambapo zaidi ya miti 1500 inatazamiwa kupandwa katika shule hiyo.

Lakini pia wananchi wa kijiji cha Kwamwande hawakusita kuonyesha furaha yao kwa uongozi wa Wilaya kwa kushiriki zoezi la upandaji wa Miti katika Shule hiyo, hayo yalibainika pale Mzee Ibrahim Chauya alipopewa nafasi ya kuzungumza.

Imetayarishwa na.

Samwel D.Mwantona ( Afisa TEHAMA)


Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mheshimiwa Sauda S.Mtondoo akizungumza na wananchi pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi Kwamwande waliojitokeza katika uzinduzi wa Wiki ya upandaji Miti Wilaya. Uzinduzi huo umefanyika shule ya Msingi Kwamwande leo tarehe 22.05.2019. Ambapo jumla ya miti 1,959,000 inatarajiwa kupandwa ndani ya Wilaya ya Kilindi.


Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili Ndg. Natus Manumbu akizungumza neno wakati wa maadhimisho ya uzinduzi wa wiki ya upandaji miti Wilaya ya Kilindi. Maadhimisho hayo yamefanyika katika Shule ya Msingi Kwamwande leo tarehe 22.05.2019.



Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi Ndg. Edward Masona akipanda mti katika shule ya Msingi Kwamwande, Siku ya uzinduzi wa wiki ya upandaji Miti Wilaya ya Kilindi. Maadhimisho hayo yamefanyika katika Shule ya Msingi Kwamwande leo tarehe 22.05.2019.

Mkuu wa wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda S.Mtondoo (katikati) akifuatilia uwasilishaji wa mada zilizokuwa zikitolewa wakati wa uzinduzi wa juma la upandaji miti Wilaya ya Kilindi. Wengine katika picha ni Diwani wa Kata ya Bokwa Mhe. Idrisa Mgaza (kulia kwake) na Kaimu Mkurugezi wa Halmashauri Ndg. Edward Masona (kushoto kwake). Maadhimisho hayo yamefanyika katika Shule ya Msingi Kwamwande leo tarehe 22.05.2019.



Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kwamwande na Wananchi walioshiriki uzinduzi wa juma la upandaji miti Wilaya ya Kilindi. Maadhimisho hayo yamefanyika katika Shule ya Msingi Kwamwande leo tarehe 22.05.2019.

Afisa Uchaguzi Wilaya ya Kilindi Ndg. Clovis Mrutu akielezea faida za upandaji miti mara baada ya kupanda mti huo katika shule ya Msingi Kwamwande siku ya uzinduzi wa juma la upandaji miti Wilaya Kilindi. Maadhimisho hayo yamefanyika katika Shule ya Msingi Kwamwande leo tarehe 22.05.2019.

Mwananchi kutoka kijiji cha Kwamwande akishiriki zoezi la upandaji miti kwa kupanda mti katika Shule ya Msingi Kwamwande siku ya uzinduzi wa juma la upandaji miti. Maadhimisho hayo yamefanyika katika Shule ya Msingi Kwamwande leo tarehe 22.05.2019.

Baadhi ya wazee wa kijiji cha Kwamwande wakishirikiana kupanda mti katika uzinduzi wa juma la upandaji miti Wilaya ya Kilindi. Maadhimisho hayo yamefanyika katika Shule ya Msingi Kwamwande leo tarehe 22.05.2019.

Diwani wa Kata ya Bokwa Mhe. Idrisa Mgaza akizungumza jambo wakati wa uzinduzi wa juma la upandaji miti Wilaya ya Kilindi. Maadhimisho hayo yamefanyika katika Shule ya Msingi Kwamwande leo tarehe 22.05.2019.


Wanafunzi wakionyesha furaha yao mara baada ya miti kupandwa katika shule yao siku ya uzinduzi wa juma la upandaji Miti Wilaya ya Kilindi, huku Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda S.Mtondoo (aliyesimama nyuma mwenye ushungi mwekundu) pamoja na baadhi ya viongozi wakishuhudia tendo hilo. Maadhimisho hayo yamefanyika katika Shule ya Msingi Kwamwande leo tarehe 22.05.2019.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI WILAYA YA KILINDI KWAAJILI YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA MWAKA 2024 September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA ZA JESHI LA MAGEREZA February 01, 2024
  • TANGAZO LA CHAGUZI NDOGO ZA UDIWANI KUTOKA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZA (NEC) February 17, 2024
  • TAASISI YA MO DEWJI KUTOA HUDUMA ZA MATIBABU YA MACHO NA KUMUONA DAKTARI BINGWA WA AKINA MAMA BURE WILAYANI KILINDI June 23, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KILINDI YAPOKEA FEDHA KIASI CHA SHILINGI MILIONI 632 ZA MIRADI

    June 22, 2025
  • MRADI WA MAJI KWAMALIGWA-GITU KUNUFAISHA WAKAZI 36,263

    June 17, 2025
  • MWENGE WA UHURU WILAYANI KILINDI WAPITIA MIRADI YENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 7.9

    June 10, 2025
  • MH: WAZIRI ULEGA AFANYA ZIARA NA KUKAGUA UJENZI WA BARABARA WILAYA KILINDI

    January 05, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda S.Mtondoo alipotembelea Mgodi wa Dhahabu wa Seita
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Hati ya Mishahara
  • SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO TANZANIA, 2015
  • SERA YA TEHAMA YA TAIFA YA MWAKA 2016
  • SHERIA YA MIAMALA YA KIELEKTRONIKI YA MWAKA 2015
  • SHERIA YA MAWASILIANO YA KIELEKTRONIKI NA POSTA 2010
  • KITENGO CHA MUITIKIO WA DHARURA WA MATUKIO YA MITANDAONI
  • Mfumo wa Mpango na Bajeti
  • Mfumo wa ffars
  • Mwongozo wa Kutumia Mfumo wa FFARS

Tovuti Nyingine

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • Baraza la Taifa la Elimu ya kiufundi
  • Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala bora
  • Tovuti ya Ikulu
  • TUME YA TAIFA YA UKIMWI TANZANIA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Copyright ©2018 Kilindi DC . All rights reserved.