• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kilindi District Council
Kilindi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara
        • Elimu Msingi
        • Elimu Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maendeleo ya Jamii
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Ardhi na Maliasili
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Shughuli za Mifugo na Uvuvi
    • Shughuri za Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji na Umwagiliaji
    • Huduma za Kilimo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu na Majukumu yake
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Mradi wa Maji
      • Miradi ya Afya
    • Miradi inayoendelea
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
    • Miradi iliyokamilika
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video Mbalimbali

WAKAZI WILAYANI KILINDI WATAKIWA KUSHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI YA MWAKA 2022

Posted on: August 21st, 2022

Wakazi wa Wilaya Kilindi wametakiwa kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 ili kuwezesha kupatikana Takwimu sahihi kwa ajili ya kupanga mipango ya maendeleo kwa usahihi

Wito huo umetolewa leo na Mh:Abel Yeji Busalama ambaye ni Mkuu wa wilaya Kilindi katika viwanja vya shule ya sekondari ya Seuta iliyopo katika kata ya Songe, wakati wa maandamano ya kuhamasisha  wananchi kushiriki Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022 wilayani Kilindi.

Alisema kupitia Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022 wakazi wa Wilaya Kilindi wataweza kupat mgao wa fursa za kimaendelo kulingana na idadi ya watu wake na hivyo kuwezesha jamii kunufaika na hatimaye kupata maendeleo stahiki

Alisema Taifa la Tanzania lilifanya Sensa mwaka 2012 na tangu kipindi hicho Wilaya Kilindi imepitia mabadiliko mbalimbali ikiwemo ongezeko la wageni kutoka katika maeneo mbalimbali ya Tanzania kama vile waliohamia kutoka mkoa wa Arusha pamoja na wageni kutoka nje ya nchi wanaofanya shughuli mbalimbali kama za migodini.

Mh:Busalama alisema kufuatia ongezeko hili  hata mahitaji ya huduma za kijamii yameongezeka,hivyo Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022 itatoa taswira halisi ya idadi ya watu na mahitaji  yao na mambo mengine mengi ya kimaendeleo na kuwezesha serikali na wadau wake wa maendeleo kupanga mipango ya maendeleo kulingana na mahitaji ya watu waliopo.

“Takwimu za watu na nyinginezo zitakazopatikana katika zoezi la Sensa  zitawezesha Mh:Mbunge,Wah:Madiwani na wadau wengine kujenga hoja za migao ya fursa za maendelo kwa mujibu wa Takwimu sahihi”Alisema Mh:Busalama na kusisitiza wakazi  Wilayani hapa kuhamasishana kushiriki zoezi  la Sensa  kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Alisema hakuna haja ya kuficha jambo wakati kaya itakapotakiwa kutoa taarifa zake kwa karani wa Sensa kwani taarifa zote ni siri na Sensa haihitaji jina wala dini ya mtu,hitaji la Sensa ni Takwimu  na taarifa mbalimbali za kimaendeleo ambazo zitaulizwa  wakati wa zoezi na kuwataka wakuu wa kaya kutowaficha walemavu,wazee na hata wagonjwa wa akili kwani nao ni sehemu ya jamii na wana mahitaji yao ya msingi yanayopaswa kuwekwa katika mipango ya maendeleo.

Akizungumza katika uhamasishaji huo Mbunge wa Jimbo la Kilindi Mh:Omary Kigua alisema Sensa ni muhimu katika Taifa lolote duniani, ndiyo maana serikali ya Tanzania ilitenga zaidi ya Tsh Bilioni 370 kwa ajili ya zoezi hili muhimu na kwamba hakuna nchi yeyote inayoweza kupanga mipango ya maendeleo bila kuwa na Takwimu sahihi za wananchi wake na mahitaji yao.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Kilindi Mh:Idrisa Mgaza akizungumzia Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022 alisema mkazi yeyote wa Wilaya Kilindi anatakiwa kuhesabiwa na yeyote ambaye hatahesabiwa atakuwa hajaitendea haki na itakuwa sawa na mtu aliyeidhulumu Wilaya kwa kuikosesha kupatikana takwimu sahihi.

Akizungumzia maandalizi Mratibu wa Sensa Wilaya Kilindi Thadeus Kway alisema kila kitu kipo tayari kwa ajili ya Sensa  ya Watu na Makazi  mwaka 2022 itakayofanyika katika Wilaya Kilindi ambayo ina kata 21,vijiji 102 na vitongoji 608 na kuwataka wakazi wilayani hapa kushiriki na kuhakikisha kila mtu katika kaya anahesabiwa.

Baadhi ya Viongozi wengine walioshiriki  maandamano ya kuhamasisha Sensa  yaliyoongozwa na Mh:Mkuu wa Wilaya Kilindi ni Katibu Tawala Wilaya,Katibu wa CCM Wilaya,Mkurugenzi Mtendaji na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya Kilindi na wananchi mbalimbali.

NA: MODI MNGUMI

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI WILAYA YA KILINDI KWAAJILI YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA MWAKA 2024 September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA ZA JESHI LA MAGEREZA February 01, 2024
  • TANGAZO LA CHAGUZI NDOGO ZA UDIWANI KUTOKA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZA (NEC) February 17, 2024
  • TAASISI YA MO DEWJI KUTOA HUDUMA ZA MATIBABU YA MACHO NA KUMUONA DAKTARI BINGWA WA AKINA MAMA BURE WILAYANI KILINDI June 23, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KILINDI YAPOKEA FEDHA KIASI CHA SHILINGI MILIONI 632 ZA MIRADI

    June 22, 2025
  • MRADI WA MAJI KWAMALIGWA-GITU KUNUFAISHA WAKAZI 36,263

    June 17, 2025
  • MWENGE WA UHURU WILAYANI KILINDI WAPITIA MIRADI YENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 7.9

    June 10, 2025
  • MH: WAZIRI ULEGA AFANYA ZIARA NA KUKAGUA UJENZI WA BARABARA WILAYA KILINDI

    January 05, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda S.Mtondoo alipotembelea Mgodi wa Dhahabu wa Seita
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Hati ya Mishahara
  • SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO TANZANIA, 2015
  • SERA YA TEHAMA YA TAIFA YA MWAKA 2016
  • SHERIA YA MIAMALA YA KIELEKTRONIKI YA MWAKA 2015
  • SHERIA YA MAWASILIANO YA KIELEKTRONIKI NA POSTA 2010
  • KITENGO CHA MUITIKIO WA DHARURA WA MATUKIO YA MITANDAONI
  • Mfumo wa Mpango na Bajeti
  • Mfumo wa ffars
  • Mwongozo wa Kutumia Mfumo wa FFARS

Tovuti Nyingine

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • Baraza la Taifa la Elimu ya kiufundi
  • Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala bora
  • Tovuti ya Ikulu
  • TUME YA TAIFA YA UKIMWI TANZANIA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Copyright ©2018 Kilindi DC . All rights reserved.