• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kilindi District Council
Kilindi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara
        • Elimu Msingi
        • Elimu Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maendeleo ya Jamii
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Ardhi na Maliasili
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Shughuli za Mifugo na Uvuvi
    • Shughuri za Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji na Umwagiliaji
    • Huduma za Kilimo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu na Majukumu yake
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Mradi wa Maji
      • Miradi ya Afya
    • Miradi inayoendelea
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
    • Miradi iliyokamilika
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video Mbalimbali

Mhe.DC KILINDI ahamasisha umuhimu wa Hatimiliki Za Ardhi kwa wananchi

Posted on: December 16th, 2020

Mkuu wa wilaya Kilindi Mh:Sauda Mtondoo amewataka viongozi wilayani hapa kuwahamasisha na kuwaelimisha wananchi  kuhusu umuhimu wa kuwa na hatimiliki za ardhi.

Mh:Mtondoo alitoa wito huo jana wakati akikabidhi hatimiliki za ardhi  kwa wananchi  na taasisi za serikali wakati wa  hafla fupi ya makabidhiano ya hati hizo iliyofanyika katika ofisi za makao makuu ya Halmashauri ya wilaya Kilindi.

Alisema hivi sasa huduma za upatikanaji wa hati za umiliki wa ardhi zimesogezwa karibu na wananchi uamuzi ambao ulifanywa na serikali kwa lengo la kusogeza huduma kwa wananchi baada ya kuanzishwa kwa ofisi za ardhi ngazi za mikoa,hivyo ni wajibu wa viongozi wilayani hapa kuhamasisha na kuelimisha wananchi kuchangamkia fursa hii muhimu.

“Awali wananchi ilibidi wasafiri mpaka Moshi mkoani Kilimanjaro ili kupata hati ya umiliki wa ardhi lakini sasa hatuna budi kuishukuru serikali kwa kusogeza huduma hii hapa katika mkoa wa Tanga na leo hii tunashuhudia wananchi wakikabidhiwa hati zao hapa wilayani” alisema Mh:Mkuu wa wilaya.

Alisema kwa sababu ya umbali wa kutoka  Kilindi hadi Moshi wananchi wengi walikuwa wakishindwa kufuatilia hati zao kwa sababu ya gharama za usafiri na nyinginezo na kuishukuru serikali kwa uamuzi wa kusogeza huduma katika ngazi ya mkoa.

Mh:Mtondoo alisema hati za ardhi zinaweza kutumika katika mambo mbalimbali ikiwemo kupata mikopo katika taasisi za kifedha na hatimaye kuweza kufanya shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

Akizungumza awali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya Kilindi bwana Gracian Makota aliwapongeza wananchi waliopata hati za  ardhi na kuwataka wananchi wengine kujitokeza kupata hati hizo ili kuwa wamiliki halali  wa ardhi kisheria.

Akitoa takwimu  afisa ardhi wilaya Kilindi bwana Natus Manumbu alisema jumla ya hati 49 zimeidhinishwa na kusajiliwa na Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Tanga ambapo kati ya hizo 21 ni Hati za  viwanja vya serikali na 28 ni Hati za viwanja vya wananchi.

Hafla hii fupi ilihudhuriwa na wananchi na viongozi mbalimbali kutoka wilayani na mkoani akiwemo Kamishna wa ardhi msaidizi mkoa wa Tanga bwana Tumaini Gwakisa ambae aliambatana na Viongozi waandamizi kutoka Ofisini kwake.

Modi Mngumi-Kilindi

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI WILAYA YA KILINDI KWAAJILI YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA MWAKA 2024 September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA ZA JESHI LA MAGEREZA February 01, 2024
  • TANGAZO LA CHAGUZI NDOGO ZA UDIWANI KUTOKA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZA (NEC) February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA April 17, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MH: WAZIRI ULEGA AFANYA ZIARA NA KUKAGUA UJENZI WA BARABARA WILAYA KILINDI

    January 05, 2025
  • WAKAZI WA MGERA WALIOJENGA KANDO YA MTO LUKIGULA WATAKIWA KUONDOKA

    December 20, 2024
  • JAMII ITOE KIPAUMBELE ULAJI WENYE MAKUNDI YOTE MUHIMU YA VYAKULA

    December 12, 2024
  • HALMASHAURI YA WILAYA KILINDI YATOA MIKOPO YA SHILINGI MILIONI 569,850,000.00

    November 18, 2024
  • Tazama zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda S.Mtondoo alipotembelea Mgodi wa Dhahabu wa Seita
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Hati ya Mishahara
  • SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO TANZANIA, 2015
  • SERA YA TEHAMA YA TAIFA YA MWAKA 2016
  • SHERIA YA MIAMALA YA KIELEKTRONIKI YA MWAKA 2015
  • SHERIA YA MAWASILIANO YA KIELEKTRONIKI NA POSTA 2010
  • KITENGO CHA MUITIKIO WA DHARURA WA MATUKIO YA MITANDAONI
  • Mfumo wa Mpango na Bajeti
  • Mfumo wa ffars
  • Mwongozo wa Kutumia Mfumo wa FFARS

Tovuti Nyingine

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • Baraza la Taifa la Elimu ya kiufundi
  • Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala bora
  • Tovuti ya Ikulu
  • TUME YA TAIFA YA UKIMWI TANZANIA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Copyright ©2018 Kilindi DC . All rights reserved.