• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kilindi District Council
Kilindi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara
        • Elimu Msingi
        • Elimu Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maendeleo ya Jamii
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Ardhi na Maliasili
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Shughuli za Mifugo na Uvuvi
    • Shughuri za Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji na Umwagiliaji
    • Huduma za Kilimo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu na Majukumu yake
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Mradi wa Maji
      • Miradi ya Afya
    • Miradi inayoendelea
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
    • Miradi iliyokamilika
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video Mbalimbali

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Atangaza Neema Kwa Wanafuzi Watakao Faulu Kidato Cha Nne Kilindi

Posted on: September 28th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martin Shigela jana ametoa ahadi ya Shilingi laki mbili kwa kila mwanafunzi wa kidato cha nne atakayepata ufaulu wa daraja la kwanza katika Shule ya Sekondari ya  wasichana Kilindi.

Mhe. Shigela alitoa ahadi hiyo alipofanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa madarasa katika shule hiyo, ikiwa ni kuwapa hamasa wanafunzi hao wanaotarajia kufanya mtihani wa kidato cha nne mapema mwezi Novemba. Hii ni kutokana na shule hiyo kukosa ufaulu wa daraja la kwanza katika mtihani wa Taifa kidato cha nne mwaka jana.

“Tunajipanga kuangalia ni namna gani kila mwanafunzi anaweza kuhitimu lakini si kuhitimu tu bali kuhitimu kwa ufaulu mkubwa” alisema Mhe. Shigela na kuongezea kwamba “ Kila mwanafunzi atakayepata daraja la kwanza katika mtihani wa Taifa nitampatia laki mbili bila kujali wangapi mtapata daraja hilo”.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martin Shigela akizungumza na wanafunzi wa kidatoa cha nne Shule ya Sekondari ya wasichana Wilayani Kilindi (hawapo pichani) siku ya tarehe 27/09/2018, kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda Mtondoo. Picha na Samwel Mwantona

Maneno hayo ya Mkuu wa Mkoa yalipokelewa kwa shangwe na wanafunzi hao kama ishara ya kuongeza juhudi katika masomo yao ilikupata zawadi hiyo iliyoaidiwa na kiongozi huyo wa Mkoa wa Tanga.

Hata hivyo Katibu Tawala Mkoa wa Tanga Bi. Zena Said aliwahamasisha wanafunzi hao kusoma kwa bidii kwani wataalam na viongozi wa aina mbalimbali wa kizazi kijacho  watatokana na wao, hivyo aliwaasa kuepukana na vishawishi lakini pia mambo yanayoweza kuathiri elimu yao.

Mbali na Mradi wa madarasa katika shule hiyo Mhe.Shigela alikagua Mradai wa ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Mnkonde lakini pia Mradi wa ujenzi wa maji Kata ya Msanja (Mradi wa Kwinji Muungano).

Aidha  akiwa katika mradi wa Zahanati Mkuu wa Mkoa aliupongeza uongozi wa wilaya chini ya Mkuu wa Wilaya Mhe.Sauda Mtondoo kwa kushirikiana vyema na wananchi hadi kufikia hatua ya kupaua jengo hilo la Zahanati. Lakini pia alihitaji diwani wa Kata hiyo Mhe. Mkomwa kueleza changamoto, ambapo diwani huyo aliitaji msaada katika kulikamilisha jengo hilo la Zahanati.

Naye Mkuu wa Mkoa kupitia maombi ya diwani huyo aliiahidi kutoa mifuko sabini ya saruji lakini pia rangi ya kwaaji ya jengo hilo, lakini pia Katibu Tawala wa Mkoa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kilindi walichangia mifuko 30 kila mmoja ili kuunga mkono juhudi za wananchi hao.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martin Shigela akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mnkonde alipokuwa akikagua Mradi wa Zahanati ya Kijiji hicho siku ya tarehe 27/09/2018. Kulia ni Katibu Tawala Mkoa Bi. Zena Saidi na kushoto ni Mkuu wa Wilaya Mhe. Sauda Mtondoo. Picha na Samwel Mwantona

Mbali na kukagua Mirada hiyo ya maendeleo Mhe. Shigela alizindua chuo cha Ufundi Stadi ( VETA ) kilichojengwa kata ya Mabalang’a. Ambapo ujenzi  wa chuo hicho cha ufundi chini ya Ufadhili wa shirika la “World Vission” ulianza mwaka 2002 na  umegharimu zaidi ya kiasi cha Shilingi milioni 350 mpaka kukamilika kwake.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martin Shigela akiwasili katika eneo la chuo cha Ufundi Stadi ( VETA ) kilichopo kata ya Mabalang’a wilaya ya Kilindi siku ya tarehe 27/09/2018. Kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Tanga Bi. Zena Said na Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda Mtondoo. Picha Samwel Mwantona

Akiwa katika uzinduzi huo alitoa aliomba jamii inayokizunguka chuo hicho na wanakilindi wote kuitumia fursa ya uwapo wa chuo hicho vizuri kwa kuhakikisha wanapata elimu itakayowasaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Pia alikagua vikundi mbalimbali vya wajasiriamali waliojitokeza pamoja na banda la wanafunzi wa shule ya msingi waliondaa kazi mbalimbali za sanaa katika eneo hilo. Hata hivyo Mkuu wa mkoa alivutiwa sana na uzalishaji wa zao la mhogo unaofanyika katika eneo la kilindi, hii ni kutokana na aina ya mhogo uliokuwa unazaidi ya kilo 10 alionyeshwa katika banda hilo la wakulima.

Mwisho Mkuu wa Mkoa alifanya mkutano na kusikiliza kero za wananchi Kata ya Kwediboma. Katika mkutano huo wananchi nane walipata fursa ya kuuliza maswali zaidi ya ishirini  ambapo yalipata majibu ya moja kwa moja kutoka kwa Mkuu wa Mkoa pamoja na wataalam wa Halmashauri.

Katibu Tawala Wilaya ya Kilindi Bi. Warda A.Maulid akitambulisha viongozi mbalimbali waliohudhuria sherehe za uzinduzi wa Chuo cha Ufundi VETA kata ya Mabalang’a Wilaya Kilindi siku ya tarehe 27/09/2018. Picha na Samwel Mwantona

Miongoni mwa kero iliyowasilishwa na wananchi hao ilikuwa ni pamoja na upungufu wa madarasa katika shule ya msingi Uwanja wa Ndege hii ni kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi waliopo shuleni hapo. Hari ambayo ilimgusa sana Mkuu wa Mkoa na kutoa ahadi ya mabati 130 pamoja  kufanya changizo kwa viongozi wa Halmashauri na kupata pesa na vifaa vyenye jumla ya thamani zaidi ya shilingi laki nne.

Aidha Mkuu wa Mkoa aliupongeza uongozi wa Wilaya na Halmashauri chini ya Mkuu wa Wilaya  Mhe. Sauda Mtondoo kwa namna unavyotekeleza na kusimamia kazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Wilaya.

Na Mwandishi

Samwel D.Mwantona ( A/TEHAMA)  

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI WILAYA YA KILINDI KWAAJILI YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA MWAKA 2024 September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA ZA JESHI LA MAGEREZA February 01, 2024
  • TANGAZO LA CHAGUZI NDOGO ZA UDIWANI KUTOKA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZA (NEC) February 17, 2024
  • TAASISI YA MO DEWJI KUTOA HUDUMA ZA MATIBABU YA MACHO NA KUMUONA DAKTARI BINGWA WA AKINA MAMA BURE WILAYANI KILINDI June 23, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KILINDI YAPOKEA FEDHA KIASI CHA SHILINGI MILIONI 632 ZA MIRADI

    June 22, 2025
  • MRADI WA MAJI KWAMALIGWA-GITU KUNUFAISHA WAKAZI 36,263

    June 17, 2025
  • MWENGE WA UHURU WILAYANI KILINDI WAPITIA MIRADI YENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 7.9

    June 10, 2025
  • MH: WAZIRI ULEGA AFANYA ZIARA NA KUKAGUA UJENZI WA BARABARA WILAYA KILINDI

    January 05, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda S.Mtondoo alipotembelea Mgodi wa Dhahabu wa Seita
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Hati ya Mishahara
  • SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO TANZANIA, 2015
  • SERA YA TEHAMA YA TAIFA YA MWAKA 2016
  • SHERIA YA MIAMALA YA KIELEKTRONIKI YA MWAKA 2015
  • SHERIA YA MAWASILIANO YA KIELEKTRONIKI NA POSTA 2010
  • KITENGO CHA MUITIKIO WA DHARURA WA MATUKIO YA MITANDAONI
  • Mfumo wa Mpango na Bajeti
  • Mfumo wa ffars
  • Mwongozo wa Kutumia Mfumo wa FFARS

Tovuti Nyingine

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • Baraza la Taifa la Elimu ya kiufundi
  • Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala bora
  • Tovuti ya Ikulu
  • TUME YA TAIFA YA UKIMWI TANZANIA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Copyright ©2018 Kilindi DC . All rights reserved.