Mkuu wa mkoa wa Tanga Mh:Omary Mgumba amekemea vikali tabia ya baadhi ya wenyeviti wa serikali za vijiji mkoani hapa kuacha kufanya vitendo vinavyosababisha migogoro ya ardhi kwani haina manufaa kwa wananchi na badala yake imekuwa ni chanzo cha vurugu na kurudisha nyuma maendeleo
Mh:Mgumba aliyasema hayo katika ziara yake ya kikazi wakati alipokuwa akizungumza na waheshimiwa Madiwani wa Baraza la Halmashauri ya Wilaya Kilindi.
Alisema mipaka kati ya eneo moja na jingine ipo kwa ajili ya kuwapima viongozi wa serikali waliowekwa kwa ajili ya kumsaidia Mh:Rais ili kuweza kujua kazi zao walizopangiwa zinaishia wapi na sio kwa ajili ya kusababisha vurugu na kujenga chuki kwa jamii.
“Lakini viongozi wanaong’ang’ania mipaka sio viongozi wakubwa ni wenyeviti wa vijiji vyetu wanataka yale maeneo sio kwa kuwatumikia wananchi bali kuuza ardhi ya wananchi”Alisema M:Mkuu wa mkoa.
Alisema kwa mujibu wa sheria ya Ardhi Namba ya vijiji,kijiji hakina mamlaka ya kuuza zaidi ya ekari 50 na wale wote waliopata ardhi kwa kupewa na wenyeviti wa ardhi na wajumbe wake bila kupitia mkutano mkuu ardhi hiyo ni malai ya kijiji.
Alisema ni kweli hajaanza kazi anatuma salamu kama kuna mwenyekiti kaingia au yupo madarakani kwa sababu ya kuuza ardhi ya wananchi bila ridhaa ya wananchi wenyewe basi imekula kwake na kuongeza kuwa na wale wenyeviti wote wasiosoma taarifa kwa wanakijiji kila baada ya robo kwa mujibu wa sheria hao hawana nafasi kwenye uongozi wa Mh:Samia Suluhu Hassan.
Alisema viongozi wapo kwa ajili kusimamia sheria na sio kuona haki na sheria zinavunjwa ni lazima kila kiongozi asimamie wajibu ili kuwasaidia wananchi haswa wale wanyonge wanopuuzwa siku zote haki zao.
NA MODI MNGUMI KILINDI
Copyright ©2018 Kilindi DC . All rights reserved.