• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kilindi District Council
Kilindi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara
        • Elimu Msingi
        • Elimu Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maendeleo ya Jamii
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Ardhi na Maliasili
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Shughuli za Mifugo na Uvuvi
    • Shughuri za Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji na Umwagiliaji
    • Huduma za Kilimo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu na Majukumu yake
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Mradi wa Maji
      • Miradi ya Afya
    • Miradi inayoendelea
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
    • Miradi iliyokamilika
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video Mbalimbali

Wilaya Ya Kilindi Yawasha Moto Wa Michezo

Posted on: March 31st, 2019

Hii ni kauli unayoweza ukaisema baada ya Kamati ya Michezo Wilaya ya Kilindi kufanya Bonanza kubwa la michezo mbalimbali lililofanyika shule ya msingi Bokwa jana tarehe 30 March 2019.

Ambapo wananchi na Viongozi wote wa Serikali na Siasa wa Wilaya ya Kilindi wakiongozwa na Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda Mtondoo walikutana kwa pamoja katika bonanza hilo.

Aidha ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilindi kwa kushirikia na Mkurugenzi Mtendaji wameunda kamati ya michezo ya Wilaya, yenye lengo la kusimamia Michezo mbalimbali ili kusudi kuinua vipaji lakini pia kuwaunganisha vijana na wananchi wote kwa ujumla.

Tarehe 30 Machi 2019 (jana) ni siku ambayo itabakia katika kumbukumbu za wanakilindi kutokana na michezo iliyofanyika katika bonanza hilo kuvutia wengi yaani si watoto, vijana wala wazee kila mmoja alishiriki kwa nafasi yake.


Akizungumzia bonanza hilo kwa furaha Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda Mtondoo  alisema “Mikakati yetu kama Wilaya nikuona zoezi hili la michezo linaendelea si tu kwa wilaya mpaka ngazi ya Kijiji”

Aidha kamati hii iliyochini ya Mwenyekiti Bi.Warda Maulid (katibu tawala Wilaya ya Kilindi) imeanza kazi kwa kuratibu bonanza hili lenye mafanikio lililohusha timu kutoka katika tarafa nne za Wilaya ya Kilindi.

Moja ya michezo ilifanyika ni mpira wa miguu, mpira wa Pete, Mpira wa Mikono,Kuvuta kamba, Sarakasi, kukimbiza kuku. Michezo hii yote haikubagua umri wa jinsia kila mmoja alishiriki kwa nafasi yake.

Mpira wa Miguu fainali walicheza tarafa ya Kimbe na tarafa ya Kwekivu ambapo tarafa ya Kwekivu waliibuka washindi baada ya kupata penati nane kwa saba kutokana na dakika 90 kumalizika kwa sale ya bao moja kwa moja.

Katika hali isiyo ya kawaida licha ya mvua kunyesha wakati michezo ikiendelea lakini mamia ya washiriki waliendelea kubaki katika kiwanja kushuhudia michezo hiyo iliyoweza kuwaunganisha wanakilindi kuwa kitu Kimoja.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya alitumia jukwaa hilo kutoa elimu ya mapambano dhidi ya virusi vya UKIMWI, Malaria lakini pia kuwahamasisha wananchi kuhusu Uchaguzi wa Serikari za Mitaa.

Kaimu mkurugenzi wa Wilaya ya Kilindi Ndg. Edward Masona aliipongeza sana kamati kwa maandalizi mazuri lakini pia alihamasisha wananchi kwendelea kujihusisha na michezo kwakuwa kupitia michezo maadui wanaweza kukaa pamoja.

Imeandaliwa na:

Samwel D.Mwantona ( Afisa TEHAMA )


Kikundi cha Sarakasi kata ya Bokwa kikionyesha burudani wakati wa tamasha la Michezo Wilaya ya Kilindi lililofanyika Shule ya Msingi Bokwa siku ya tarehe 30 Machi 2019.


Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda Mtondoo akikagua timu ya Tarafa ya Kwekivu walipokuwa katika bonanza la Michezo Wilaya ya Kilindi lililofanyika shule ya Msingi Bokwa tarehe 30 Machi 2019.



Katibu Tawala Wilaya ya Kilindi Bi. Warda Maulidi alipokuwa akiongoza Maandamano siku ya Bonanza la Michezo Wilaya ya Kilindi lililofanyika Shule ya Msingi Bokwa tarehe 30 Machi 2019.



Diwani wa kata ya Bokwa Mhe. Idrisa Mgaza akiwa katika maandamano ya Bonanza la Michezo Wilaya ya Kilindi, lililofanyka shule ya Msingi Bokwa siku ya tarehe 30 Machi 2019.


Baadhi ya zawadi zilizoandaliwa kwa washindi wa Bonanza la Michezo Wilaya ya Kilindi lililofanyika tarehe 30 Machi 2019 shule ya msingi Bokwa.


Baadhi ya wananchi waliojitokeza katika maandamano ya Bonanza la Michezo Wilaya ya Kilindi lililofanyika Shule ya Msingi Bokwa tarehe 30 Machi 2019.



Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda Mtondoo akimpa hongera mshindi wa mchezo wa kukimbiza kuku wakati wa Bonanza la Michezo la Wilaya ya Kilindi lililofanyika Shule ya Msingi Bokwa tarehe 30 Machi 2019.


Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya kilindi Ndg. Gracian Makota akisikiliza jambo kutoka kwa Mbunge wa jimbo la Kilindi Mhe. Omary Kigua walipokuwa katika Bonanza la Michezo Wilaya ya kilindi lilipofanyika shule ya Msingi Bokwa tarehe 30 Machi 2019.


Kikosi cha Askari Mgambo kikitoa burudani ya gwalide katika Bonanza la Michezo Wilaya ya Kilindi lililofanyika Shule ya Msingi Bokwa tarehe 30 Machi 2019.

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda Mtondoo akizungumza na wananchi waliojitokeza katika Bonanza la Michezo Wilaya ya Kilindi, lililofanyika shule ya Msingi Bokwa tarehe 30 Machi 2019.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI WILAYA YA KILINDI KWAAJILI YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA MWAKA 2024 September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA ZA JESHI LA MAGEREZA February 01, 2024
  • TANGAZO LA CHAGUZI NDOGO ZA UDIWANI KUTOKA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZA (NEC) February 17, 2024
  • TAASISI YA MO DEWJI KUTOA HUDUMA ZA MATIBABU YA MACHO NA KUMUONA DAKTARI BINGWA WA AKINA MAMA BURE WILAYANI KILINDI June 23, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KILINDI YAPOKEA FEDHA KIASI CHA SHILINGI MILIONI 632 ZA MIRADI

    June 22, 2025
  • MRADI WA MAJI KWAMALIGWA-GITU KUNUFAISHA WAKAZI 36,263

    June 17, 2025
  • MWENGE WA UHURU WILAYANI KILINDI WAPITIA MIRADI YENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 7.9

    June 10, 2025
  • MH: WAZIRI ULEGA AFANYA ZIARA NA KUKAGUA UJENZI WA BARABARA WILAYA KILINDI

    January 05, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda S.Mtondoo alipotembelea Mgodi wa Dhahabu wa Seita
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Hati ya Mishahara
  • SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO TANZANIA, 2015
  • SERA YA TEHAMA YA TAIFA YA MWAKA 2016
  • SHERIA YA MIAMALA YA KIELEKTRONIKI YA MWAKA 2015
  • SHERIA YA MAWASILIANO YA KIELEKTRONIKI NA POSTA 2010
  • KITENGO CHA MUITIKIO WA DHARURA WA MATUKIO YA MITANDAONI
  • Mfumo wa Mpango na Bajeti
  • Mfumo wa ffars
  • Mwongozo wa Kutumia Mfumo wa FFARS

Tovuti Nyingine

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • Baraza la Taifa la Elimu ya kiufundi
  • Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala bora
  • Tovuti ya Ikulu
  • TUME YA TAIFA YA UKIMWI TANZANIA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Copyright ©2018 Kilindi DC . All rights reserved.