• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kilindi District Council
Kilindi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara
        • Elimu Msingi
        • Elimu Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maendeleo ya Jamii
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Ardhi na Maliasili
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Shughuli za Mifugo na Uvuvi
    • Shughuri za Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji na Umwagiliaji
    • Huduma za Kilimo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu na Majukumu yake
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya maadili
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Mradi wa Maji
      • Miradi ya Afya
    • Miradi inayoendelea
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
    • Miradi iliyokamilika
      • Huduma za Afya
      • Mradi wa Maji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video Mbalimbali

Kakakuona Aonekana Wilayani Kilindi.

Posted on: March 22nd, 2019

Mnyama adimu na mwenye mvuto, Kakakuona ameonekana katika kijiji cha Kilwa kata ya Kilwa ndani ya Wilaya ya Kilindi mnamo tarehe 14/03/2019.

Mnyama huyu ni miongoni mwa wanyama adimu na waliojizolea umaarufu mkubwa kote ulimwenguni kwa tabia yake ya kutabiri mambo mbalimbali kwa kuchagua kitu kimoja wapo kati ya vitu mbalimbali vilivyowekwa mbele yake.

Aidha Wilaya ya Kilindi imekuwa miongoni mwa wilaya chache nchini Tanzania zilizopata bahati ya kumona mnyama huyu kwa miaka miwili mfululizo. Ambapo kwa mara ya kwanza alionekana katika Kitongoji cha Matangagoja kilichopo kijiji cha Kilindi Asilia ndani ya kata ya Kilindi mwaka 2018 mwezi wa saba.

Hata hivyo alipooneka kwa mara ya kwanza katika kijiji cha Kilindi Asilia wanakijiji walimwekea mahindi, fedha na maguzi ilikubaini utabiri wake kwa maeneo yao na Wilaya kwa ujumla. Aidha mnyama huyu alielekea kwenye maguzi badala ya fedha na mahindi.

Akielezea tukio hilo Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji cha Kilindi Ndg.Ramadhani Athumani Msuluwa alisema “ Utabiri wa Kakakuona ulikuwa sahihi kwasababu msimu ule hatukupata mazao ya kutosha kutokana na mvua kubwa iliyoharibu mazao”.

Kwa awamu hii ya pili alipoonekana ndani ya kijiji cha Kilwa hakuweza kufanya utabiri wowote. Ila wananchi waliopata fursa ya kumtizama walivutiwa sana na kuitizama Wilaya ya Kilindi kuwa ni eneo lenye bahati kubwa ndani ya Tanzania kwa kupatikana mnyama huyo kwa miaka miwili mfululizo.

Lakini pia Ofisi ya Mkurugezi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi kwa kushirikiana na Jeshi la polisi kituo cha Kwediboma imekamilisha taratibu zote na kumkabidhi Mhifadhi wa wanyama pori wa Mbuga ya Sadani iliyopo Wilaya ya Pangani Mkoa wa Tanga mnamo tarehe 21/03/2019

Hii ni mara ya pili Mkurugenzi Mtendaji kufanya utaratibu huu wa kuwakabidhi wanyama pori hawa katika hifadhi ya Sadani baada ya kumkabidhi Kakakuona aliyepatikana Kijiji cha Kilindi asilia Kwa Wahifadhi hao mnamo tarehe 31/07/2019. Ikiwa ni lengo la kutunza wanyama hawa kwa vizazi vijavyo vya Taifa letu.

Kakakuona ni mnyama aliyezungukwa na magamba makubwa katika sehemu ya mwili wake hari ambayo utoa wakati mgumu kwa maadui kumshambulia kutokana na ugumu wa magamba hayo hasa pale anapojivilinga aisipo maadui.

Imeandaliwa na.

Samwel D.Mwantona (Afisa TEHAMA)

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI WILAYA YA KILINDI KWAAJILI YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA MWAKA 2024 September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA ZA JESHI LA MAGEREZA February 01, 2024
  • TANGAZO LA CHAGUZI NDOGO ZA UDIWANI KUTOKA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZA (NEC) February 17, 2024
  • TAASISI YA MO DEWJI KUTOA HUDUMA ZA MATIBABU YA MACHO NA KUMUONA DAKTARI BINGWA WA AKINA MAMA BURE WILAYANI KILINDI June 23, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KILINDI YAPOKEA FEDHA KIASI CHA SHILINGI MILIONI 632 ZA MIRADI

    June 22, 2025
  • MRADI WA MAJI KWAMALIGWA-GITU KUNUFAISHA WAKAZI 36,263

    June 17, 2025
  • MWENGE WA UHURU WILAYANI KILINDI WAPITIA MIRADI YENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 7.9

    June 10, 2025
  • MH: WAZIRI ULEGA AFANYA ZIARA NA KUKAGUA UJENZI WA BARABARA WILAYA KILINDI

    January 05, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Mhe. Sauda S.Mtondoo alipotembelea Mgodi wa Dhahabu wa Seita
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Hati ya Mishahara
  • SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO TANZANIA, 2015
  • SERA YA TEHAMA YA TAIFA YA MWAKA 2016
  • SHERIA YA MIAMALA YA KIELEKTRONIKI YA MWAKA 2015
  • SHERIA YA MAWASILIANO YA KIELEKTRONIKI NA POSTA 2010
  • KITENGO CHA MUITIKIO WA DHARURA WA MATUKIO YA MITANDAONI
  • Mfumo wa Mpango na Bajeti
  • Mfumo wa ffars
  • Mwongozo wa Kutumia Mfumo wa FFARS

Tovuti Nyingine

  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • Baraza la Taifa la Elimu ya kiufundi
  • Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala bora
  • Tovuti ya Ikulu
  • TUME YA TAIFA YA UKIMWI TANZANIA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Copyright ©2018 Kilindi DC . All rights reserved.